KiSwahili

(verse:1)

Ee Mungu nguvu yetu
Ilete baraka kwetu

Haki iwe ngao na mlinzi
Natukae na udugu

Amani na uhuru
Raha tupate na ustawi.

(verse:2)

Amkeni ndugu zetu
Tufanye sote bidii

Nasi tujitoe kwa nguvu
Nchi yetu ya Kenya

Tunayoipenda
Tuwe tayari kuilinda

(verse:3)

Natujenge taifa letu
Ee, ndio wajibu wetu

Kenya istahili heshima
Tuungane mikono

Pamoja kazini
Kila siku tuwe na shukrani