DARASA LA I
FANI |
MADA |
MADA NDOGO |
LENGO (MWANAFUNZI) |
MBINU ZA KUFUNDISHIA |
VIFAA/REJEA |
QUR'AN |
Kusoma na Kuandika Kiarabu |
- Kutambua herufi za Kiarabu
- Kusoma na kuandika herufi za Kiarabu
|
Aweze kusoma na kuandika kwa herufi za Kiarabu |
- Mwalimu awaonyeshe na kuwatamkia wanafunzi herufi mojamoja Atumie picha na kadi.
- Wanafunzi wamfuatishe Mwalimu kutamka herufi moja moja kwa wote kisha mmoja mmoja.
- Wanafunzi wafanye mazoezi ya kuandika herufi moja moja katika ardhi, ubaoni, katika karatasi ngumu, n.k.
- Mwalimu awatambulishe wanafunzi hatua kwa hatua alama za Irabu, tanwin na sakna na atoe mazoezi ya kutosha ya kusoma na kuandika herufi za Kiarabu zikiwa na alama hizo.
- Mwalimu awaonyeshe herufi moja moja inavyokuwa ikiwa inaungwa mwanzoni, katikati na mwishoni mwa neno. Abainishe herufi zisizoungika na atoe mazoezi ya kutosha ya kusoma na kuandika.
- Mwalimu awatambulishe wanafunzi alama za madda na shadda na zinavyotumika katika kusoma·
- Mwalimu atoe mazoezi mengi ya kusoma na kuandika.
|
- Ubao na chaki.
- Kadi za herufi.
- Kadi za maneno.
- Mbao/ubao
- Juzuu Amma
- Kitabu cha I (IPC).
|
Kusoma Qur’an |
Kusoma kwa ufasaha sura ya: -
- Al-Fatiha mpaka Al- A’laa
- Kuhifadhi sura hizo
- Kuandika
- Al-Fatiha
- Annas
- Al-Falaq
- Al-Ikhlas
|
- Aweze kusoma Qur’an kwa ufasaha na kuhifadhi
- Aweze kuandika Al-Fatiha, Annas, Alfalaq na al-Ikhlas
|
- Mwalimu awasomee wanafunzi sura huku wakisikiliza kisha awaamuru kusoma katika kundi kisha mmoja mmoja.
- Mwalimu awawezeshe wanafunzi kuhifadhi kwa kumfuatisha bila kuangalia kitabuni kwa kundi na kisha mmoja mmoja.
- Mwalimu aandike ubaoni sura anayosomesha.
- Mwalimu awaamuru wanafunzi kuandika al-Fatiha, annas, Al-Falaq na Ikhlas
|
- Ubao na chaki.
- Vibao vya wanafunzi.
- Radio kaseti.
- Kitabu cha I (IPC).
|
TAWHIID |
Kuwepo kwa Allah (S.W.). |
Allah ni muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo. |
Aweze kupambanua kuwepo kwa Allah (S. W.) kutokana na mazingira yake. |
Mwalimu awaulize wanafunzi maswali yatakayowapelekea kuyakinisha kuwepo kwa Allah (S. W.) kwa kutumia mazingira yao |
- Jua.
- Mwezi.
- Nyota.
- Mawingu.
- Kitabu cha I (IPC).
|
FIQ-H |
Nguzo za Uislamu |
- Kutoa Shahada
- Kusimamisha Swala
- Kutoa zaka
- Kufunga Ramadhani
- Kuhiji Makka kwa mwenye uwezo.
|
Aweze kutaja nguzo za Uislamu. |
- Mwalimu ataje nguzo tano – moja moja kisha wanafunzi wamfuatishie kwa kundi kisha mmoja mmoja. Atumie Hadithi “Buniyal Islamu alaa khamsin….”.
-
- Wanafunzi wenyewe wataje nguzo tano katika kundi, kisha mmoja mmoja.
|
- Picha ya nyumba
-
- Yenye nguzo tano
- Kitabu cha I (IPC)
|
Shahada |
- Kutamka na kuandika Shahada
- Kutafsiri Shahada
|
Aweze kutamka na kuandika shahada Aweze kutafsiri shahada |
- Mwalimu awawezeshe wanafunzi kutamka, kuandika na kutafsiri shahada mbili kwa kuwazoesha kutamka na kuandika shahada na tafsiri yake
- Mwalimu awafahamishe wanafunzi kuwa maana ya shahada ni kufuata maamrisho na makatazo yote ya Allah (S.W.) na Mtume wake.
- Mwalimu abainishe maamrisho na makatazo ya Allah na Mtume wake kulingana na umri wa wanafunzi.
|
Kitabu cha I (IPC) |
Najsi na namna ya kujitwaha-risha |
- Vitu vilivyonajisi.
- Namna ya kujitwaharisha kutokana na najisi.
- Adabu za kwenda haja.
- Kujitwaharisha baada ya kwenda haja
|
Aweze kujua najisi na namna ya kujitwaha-risha. |
- Mwalimu awatajie wanafunzi vitu vilivyo najisi – kimoja kimoja kulingana na uzoefu wa mazingira ya wanafunzi kama vile choo kikubwa na kidogo, damu, matapishi, mzoga, n.k.
- Mwalimu awaelekeze wanafunzi kwa vitendo namna ya kuondoa najisi kwenye mwili, nguo, na mswala kisha awape wanafunzi mazoezi.
- Mwalimu awaeleze wanafunzi kwa vitendo namna ya kujisaidia na kujitwaharisha kwa maji, mawe, karatasi, n.k.
|
- Picha husika
- Rejea kitabu cha I (IPC)
|
Kutawadha |
- Namna ya kutawadha
- Yanayotengua udhu
|
- Aweze kutawadha
- Aweze kutaja yanayotengua udhu
|
- Mwalimu awaelekeze wanafunzi kutawadha kwa vitendo na awape wanafunzi mazoezi ya kutawadha mmoja mmoja mbele ya darasa.
- Aorodheshe ubaoni yale yanayotengua udhu na kuwataka wanafunzi wayarudie.
|
- Ndoo ya maji
- Makopo
- Kata, n. k.
|
AKHLAQ |
Usafi |
- Kutwaharika na najisi nguoni na mwilini
- Usafi wa mwili, kuoga, kuchana, kusuka, kukata kucha, n.k.
- Usafi wa nguo: kufua, kupiga pasi,
- Faida za usafi
|
Ajue kuwa usafi ni sehemu ya Uislamu |
- Kwa njia ya maelekezo na kumuuliza maswali mwalimu awafahamishe wanafunzi umuhimu na faida ya usafi.
- Mwalimu awaelekeze wanafunzi kwa vitendo namna ya kupiga mswaki, kukoga, kuchana nywele, kufua, kupiga pasi, n. k.
- Mwalimu kila mara awakague wanafunzi kwa usafi na unadhifu wa mwili na nguo.
- Awafahamishe wanafunzi faida za usafi na hasara za uchafu.
|
- Nguo chafu na safi.
- Miswaki
- Sabuni
- Kitana
- Kikata kucha n. k.
- Rejea picha kitabu cha I (IPC)
|
Adabu za kula. |
- Kunawa kabla ya kuanza kula
- Kuanza kula kwa Bismillah
- Utulivu wakati wa kula na heshima kwa unaokula nao
- Adabu za kula katika kundi
- Kula kwa kiasi
- Kumaliza kula kwa kumshukuru Allah (S. W.) na aliyeandaa chakula
- Usafi baada ya kula
|
Aweze kula kwa kuzingatia Sunnah |
- Mwalimu awafahamishe wanafunzi vyakula vya halali akizingatia umri wao.
- Kwa njia ya maelekezo na kuuliza maswali mwalimu awafahamishe wanafunzi vyakula vizuri vinavyokamilisha mlo na umuhimu wake katika mwili kulingana na umri wao
- Mwalimu awafahamishe wanafunzi kwa vitendo namna ya kula kwa taratibu za Kiislamu
|
- Chakula
- Ndoo ya maji
- Ndoo tupu
- Glasi za maji, n.k.
- Rejea picha kitabu cha I (IPC)
|
Michezo |
- Kucheza katika maeneo yanayokubalika.
- Kujiepusha na michezo mibaya ya uharibifu.
- Kucheza na watoto wenye maadili mema na kujiepusha na watoto wabaya.
|
Afahamu michazo na uchezaji unaokubaliana na maadili ya Kiislamu. |
- Awafahamishe wanafunzi michezo na uchezaji unaofaa na faida zake.
- Awabainishie wanafunzi michezo mibaya na awatahadharishe wanafunzi kwa kuonyesha ubaya na hasara za michezo hiyo.
|
Kitabu cha I (IPC) |
TAREKH |
Mitume wa Allah (S. W.) |
- Mitume 25 iliyotajwa katika Qur-an.
- Mitume wote wamekuja kuufundisha Uislamu.
|
Afahamu kuwa Mitume wote wamekuja kufundisha Uislamu. |
- Mwalimu ataje majina ya Mitume 25 na kuwataka wanafunzi wamfuatishe.
- Aorodheshe majina 25 kwenye ubao na kuwaamuru wanafunzi kuandika.
- Asisitize kwa wanafunzi kuwa Mitume wote wamekuja kufundisha Uislamu.
|
Kitabu cha I (IPC) |
Muhtasari huu umetayarishwa na Islamic Propagation Centre, S. L. P. 55105, Dar es salaam, Tanzania