DARASA LA III
FANI |
MADA |
MADA NDOGO |
LENGO (MWANAFUNZI) |
MBINU ZA KUFUNDISHIA |
VIFAA/REJEA |
QUR'AN |
Kusoma, kuhifadhi na kutoa ujumbe wa sura zilizochaguliwa |
- Hukumu za usomaji Qur-an.
- Idh-hari, Id-gham, Ikh-fai, Iqlab.
- Kuhifadhi sura zifuatazo: -
Al-Mursalaat hadi Al-Jinn - Tafsiri ya sura zifuatazo: -
An-Nabaa mpaka Atw-Twaariq.
|
- Aweze kutambua na kutumia hukumu zote za Qur-an.
- Ahifadhi Qur-an na aweze kutoa ujumbe sura zilizochaguliwa.
|
- Mwalimu asome sura hizo kwa utaratibu na ufasaha.
- Awape wanafunzi fursa ya kumfuatishia kwa darasa.
- Awape wanafunzi kazi ya kuandika kila sura katika daftari na kuihifadhi.
- Awape tafsiri na ujumbe wa sura hizo kwa maelezo na kuwaandikia ubaoni na kuwamuru kunakili.
|
- Qur-an na tafsiri ya Al-Farsy.
- Kitabu cha III (IPC)
|
TAWHIID |
Nguzo za Imani. |
- Katika Qur-an (2:285), n.k.
- Katika Hadithi.
|
Afahamu nguzo za Imani kwa mpangilio. |
- Mwalimu asome aya na hadithi zinazobainisha nguzo za Imani na aziandike ubaoni na tafsiri yake.
- Wanafunzi wasome kwa kumfuatisha mwalimu na waandike katika madaftari yao.
|
Kitabu cha III (IPC) |
Kuwepo Allah (S. W.) |
Kuwepo kwa mwanaadamu ni dalili ya kuwapo Allah (S. W.) ukizingatia: -
- Umbile lake.
- Uhai wake.
- Makuzi yake.
- Usingizi wake.
- Kufa kwake.
- Tofauti ya lugha, rangi na makabila .
|
- Aweze kumtambua Allah (S. W.) kutokana na mwanadamu.
- Kumuwezesha kumuogopa na kumtii Allah (S. W.) inavyostahiki.
| - Mwalimu aulize maswali yote yanayowapelekea wanafunzi watambue kuwepo kwa Allah (S. W.) kutokana na nafsi ya mwanadamu.
- Mwalimu kwa njia ya maswali na maelezo awafahamishe wanafunzi kuwa wanawajibika kumtii Allah (S. W.) na kumtumikia inavyostahiki kwa kufuata maamrisho yake na kuacha makatazo yake.
|
Kitabu cha III (IPC) |
FIQH |
Sharti za Swala |
- Twahara.
- Stara.
- Kuchunga nyakati za Swala.
- Kuelekea Qibla.
|
Aweze kutekeleza masharti yote ya Swala. |
- Mwalimu asomeshe kwa vitendo mipaka ya stara na namna ya kujisitiri.
- Awape wanafunzi mazoezi ya kujisitiri.
- Mwalimu afanye marudio ya darasa la pili katika Twahara, kuchunga wakati na kuelekea Qibla.
|
- Nguo za stara kulingana na umri wa watoto.
- Kitabu cha II (IPC)
- Kitabu cha III (IPC)
|
Kuswali. |
- Nguzo na Sunna za Swala.
- Yanayobatilisha Swala.
|
Aweze kuswali vilivyo. |
- Awatafsiriye kwa kuandika ubaoni visomo vyote vya Swala.
- Awaonyeshe wanafunzi namna ya kuswali kwa unyenyekevu.
|
Kitabu cha III (IPC) |
AKHLAQ |
Tabia njema. |
- Usafi.
- Kuishi Kiislamu saa 24.
|
- Awe msafi.
- Awe na mwenendo wa Kiislamu.
|
- Mwalimu asisitize kwa Aya na Hadithi umuhimu wa usafi.
-
- Awaelekeze wanafunzi namna watakavyoweza kuishi Kiislamu katika saa 24 kwa kurejea Hadithi sahihi.
|
Kitabu cha III (IPC) |
TAREKH |
Historia ya Uislam wakati wa Mtume Muhammad (S. A. W.) |
- Kupewa Utume.
- Wahy wa kwanza na ujumbe wake.
- Kubalighisha Uislamu.
- Upinzani alioupata Makkah.
- Mateso kwa Waislamu.
- Kuhamia Madina.
|
Aweze kueleza namna Mtume (S. A. W.) alivyoanza kuhuisha Uislamu na mafunzo tunayopata kutokana na kipindi hiki cha historia. |
- Mwalimu awahadhithie wanafunzi historia ya Mtume (S. A. W.) tangu kupewa Utume mpaka kuhamia Madinah hatua kwa hatua.
- Mwalimu abainishe mafunzo yanayopatikana katika kila hatua kulingana na umri wa wanafunzi.
|
Kitabu cha III (IPC) |
Muhtasari huu umetayarishwa na Islamic Propagation Centre, S. L. P. 55105, Dar es salaam, Tanzania