Bismillahir Rahmaanir Rahim

MUHTASARI WA ELIMU YA DINI YA KIISLAMU KWA MADRASA NA SHULE ZA MSINGI

DARASA LA IV
FANI MADA MADA NDOGO LENGO (MWANAFUNZI) MBINU ZA KUFUNDISHIA VIFAA/REJEA
QUR'AN Kusoma.
  • Ahkai – marudio darasa la III
  • Kuhifadhi na tafsiri ya sura zifuatazo: -
    Tafsiri ya Surat Al-Mursalaat, al-Jinn
  • Ujumbe wa sura zifuatazo: -
    Al-Fatiha mpaka Al-zilzal
  • Aweze kusoma Qur-an vilivyo.
  • Ahifadhi na kutafsiri Qur-an na apate ujumbe uliomo na aweze kuufuata
  • Mwalimu asome kila sura mbele ya darasa kwa utaratibu na ufasaha na awape wanafunzi fursa ya kumfuatisha.
  • Wanafunzi waandike kila sura katika madaftari yao na kuhifadhi.
  • Atoe tafsiri na ujumbe wa kila sura na kuwapa wanafunzi mazoezi ya kutafsiri na kubainisha ujumbe.
  • Aandike tafsiri na ujumbe wa kila sura ubaoni na wanafunzi wanakili madaftarini.
Kitabu cha IV (IPC)
TAWHIID Kumuamini Allah (S. W.)
  • Sifa za Allah (S. W.) katika Qur-an na Hadith.
  • Matumizi ya sifa za Allah katika kuomba dua.
  • Maana ya kumuamini Allah (S. W.)
Aweze kumuamini Allah (S. W.) ipasavyo na asimshirikishe na chochote.
  • Mwalimu awasomee na kuwaandikia ubaoni majina 99 ya Allah (S. W.) kama yalivyobainishwa katika Hadith na kuwaamuru waandike.
  • Kisha arejee sura na aya mbalimbali zinazotaja baadhi ya sifa za Allah kwa mfululizo kama aya (2:225), (57:1-6), (59:22-24), (112:1-4)
Kitabu cha IV (IPC)
FIQ-H Kusimamisha Swala
  • Kujitwaharisha kwa tayammamu.
  • Maana ya kusimamisha Swala.
  • Sijidatis-Sahau.
  • Sijida-tilawat.
  • Unyenyekevu katika Swala.
  • Swala ya jamaa.
  • Dua na dhikiri baada ya Swala.
  • Aweze kutayamamu.
  • Aweze kueleza maana ya kusimamisha Swala.
  • Aweze kuleta sijidatis –Sahau na Tilawat.
  • Aweze kusimamisha Swala ya jamaa.
  • Aweze kuleta dua na dhikiri baada ya Swala.
  • Mwalimu aelezee kinadharia na matendo namna ya kutayamamu.
  • Awaelekeze wanafunzi kwa matendo namna ya kuleta sijidatis-sahu na tilawat.
  • Awaelekeze kwa matendo namna ya kusimama kwenye Swala ya jamaa.
  • Mwalimu awaelekeze wanafunzi namna ya kufanya ili waweze kunyenyekea katika Swala.
  • Awasomee dua na dhikiri na kuwaimbisha na kisha kuwaandikia ubaoni na kuwaamuru wanakili.
Kitabu cha IV (IPC)
Zakat
  • Maana ya Zakat.
  • Wanaopaswa kutoa Zakat.
  • Vitu vinavyotolewa Zakat na viwango vyake.
  • Wanaostahiki kupewa Zakat.
Aweze kueleza maana ya Zakat, utoaji wake na mgawanyo wake. Awafahamishe maana ya Zakat, wanaopaswa kutoa, vitu vinavyotolewa Zakat na viwango vyake na wanaostahili kupewa Zakat kwa kutumia aya za Qur-an na Hadithi. Kitabu cha IV (IPC)
Funga ya Ramadhani.
  • Amri ya funga ya Ramadhani (2:183).
  • Wanaolazimika kufunga.
  • Wanaoruhusiwa kufunga.
  • Wanaoruhusiwa kula na kulipa baadaye.
  • Nia ya kufunga.
  • Maana ya kufunga.
  • Tabia anayotakiwa awe nayo mfungaji.
  • Yanayobatilisha funga.
Aweze kufunga ipasavyo.
  • Mwalimu asome na kuandika ubaoni aya (2:183) juu ya funga.
  • Mwalimu abainishe kwa maelezo na kuandika ubaoni wanaolazimika kufunga, wenye kuruhusiwa na kulipa baadaye kwa kurejea Qur-an (2:184-185), namna ya kufunga, tabia ya mfungaji na yanayobatilisha funga.
Kitabu cha IV (IPC).
AKHLAQ Mavazi ya Kiislamu
  • Lengo la vazi (7:26-27).
  • Vazi la mwanaume na mwanamke.
  • Faida ya Hijab (33:59).
Aweze kujisitiri Kiislamu.
  • Mwalimu awafahamishe wanafunzi lengo la vazi kwa kurejea Qur-an (7:26-27) na asisitize faida na umuhimu wa kujisitiri – (33:59).
  • Mwalimu aonyeshe kwa vielelezo namna ya kujisitiri Kiislamu kwa wanaume na wanawake.
Kitabu cha IV (IPC)
Michezo
  • Michezo inayoruhusiwa katika Uislamu.
  • Michezo iliyoharamishwa.
  • Michezo ya laghwi.
Aweze kushiriki katika michezo iliyoruhusiwa na kujiepusha na michezo haramu na ile ya laghwi.
  • Mwalimu abainishe michezo inayokubalika katika Uislamu.
  • Mwalimu aainishe michezo haramu na michezo ya Laghwi.
  • Mwalimu asisitize umuhimu wa kushiriki katika michezo yenye manufaa kwa vijana.
Kitabu cha IV (IPC).
TAREKH Historia ya Uislam wakati wa Mtume (S. A. W) kipindi cha Madinah.
  • Mtume (S. A. W) kuunda umma wa Kiislamu.
  • Upinzani Dhidi ya Dola ya Kiislamu.
  • Mkataba wa Hudaibiya na matunda yake.
  • Kukombolewa Makkah.
  • Msafara wa Tabuuk.
  • Kusilimu Waislamu makundi kwa makundi.
  • Hija ya kuaga.
  • Kutawafu Mtume.
Aweze kueleza namna Mtume (S. A. W) alivyosimamisha Dola ya Kiislamu Madinah, namna alivyoihami na kuufanya Uislamu kuwa juu ya dini zote.
  • Mwalimu aeleze hatua kwa hatua namna Mtume (S. A. W) alivyosimamisha Dola ya Kiislamu Madinah na kuufanya Uislamu kuwa juu ya Dini zote.
  • Mwalimu atoe mazingatio tunayopata hivi leo.
Kitabu cha IV (IPC)

Muhtasari kwa madarasa mengine

Home Darasa la Kwanza Darasa la Pili Darasa la Tatu Darasa la Tano Darasa la Sita Darasa la Saba

Muhtasari huu umetayarishwa na Islamic Propagation Centre, S. L. P. 55105, Dar es salaam, Tanzania