Bismillahir Rahmaanir Rahim

MUHTASARI WA ELIMU YA DINI YA KIISLAMU KWA MADRASA NA SHULE ZA MSINGI

DARASA LA VII
FANI MADA MADA NDOGO LENGO (MWANAFUNZI) MBINU ZA KUFUNDISHIA VIFAA/REJEA
QUR-AN Kusoma, kutafsiri na kuhifadhi. Kuhifadhi, kutafsiri sura au aya zifuatazo (Rejea Msahafu wa tafsiri): -
  • Al-Baqara (2); 1-20, 183-188, 254-257, 284-286.
  • Al-Imraan (3): 102-120, 190-200.
  • An-Nisaa (4): 11-13.
  • Al-Kahf(18): 1-31.
  • Al-Muuminuun (23): 63-77.
  • Luqman (31): 1-34.
  • Ahzaab (33): 9-27.
  • Haamiim Sajda (41).
  • Al-Fatih (48): Yote.
Ahifadhi Qur-an, ajue ujumbe unaopatikana na awe tayari kuufuata.
  • Mwalimu asome kila sura huku wanafunzi wakimfuatisha kisha waandike sura au aya hizo madaftarini mwao na kuzihifadhi.
  • Atoe tafsiri na ujumbe wa kila sura au aya kwa maelezo na kuandika ubaoni, kisha wanafunzi wanakili madaftarini mwao.
Kitabu cha VII (IPC).
HADITH Historia ya kukusanywa na kuhifadhiwa Hadith.
  • Kuhifadhiwa Hadithi.
  • Historia ya uandishi wa Hadithi wakati wa Mtume
  • Maswahaba.
  • Taabiina.
  • Tabii-Taabiina.
Aweze kueleza vilivyopatikana vitabu vya Hadithi Sahihi.
  • Mwalimu awafahamishe wanafunzi utaratibu uliotumika katika kuhifadhi Hadithi.
  • Aeleze kwa muhtasari historia ya kuandikwa Hadithi kwa kuwataja Maimam walioshughulika na uandishi wa Hadithi na historia ya maisha yao kwa ufupi.
Kitabu cha VII (IPC)
Uchambuzi wa Hadithi.
  • Migawanyiko ya Hadithi.
  • Vigezo vya Hadith Sahihi.
Aweze kutambua Hadithi Sahihi.
  • Mwalimu abainishe migawanyiko yote ya Hadith kama vile Nabawiy, Qudus, Sahihi, Hasan, Dhaifu, Maudhuu, n.k.
  • Abainishe vigezo vyote vya Hadithi sahihi kwa kuzingatia Matini na Isnad ya Hadithi.
Kitabu cha VII (IPC)
TAWHIID Imani ya Kiislamu
  • Maana ya kuamini katika Uislamu.
  • Muumini wa kweli.
  • Maana ya kuamini kila kipengele cha nguzo za Imani.
Aweze kuwa muumini wa kweli.
  • Mwalimu aeleze maana ya imani kilugha na kiistilah.
  • Kwa kurejea Hadithi abainishe vipengele sita vya nguzo za Imani na wanafunzi wanukuu Hadithi hiyo.
  • Kwa kurejea Qur-an na Hadith aonyeshe ni ipi tabia ya muumini wa kweli wa kila kipengele cha Imani.
Kitabu cha VII (IPC)
FIQ-H Maana ya Dini.
  • Maana ya dini katika Uislamu.
  • Kila mtu anayo dini.
  • Hakuna maisha ya dini na dunia.
  • Aina kuu za dini.
Aweze kueleza maana ya dini na kuwa kila mtu ana dini.
  • Awafahamishe wanafunzi maana ya dini kwa kurejea Qur-an na Hadithi na abainishe kutokana na maana hiyo kuwa kila mwanaadamu anafuata dini moja au nyingine.
  • Kwa kutumia Qur-an aonyeshe kuwa Ukafiri, Ushirikina, Utawa na Uislamu ni dini.
  • Asisitize kuwa kwa mujibu wa Qur-an Uislamu ndio dini sahihi.
Kitabu cha VII (IPC)
Ibada.
  • Maana ya Ibada.
  • Lengo la kuumbwa binadamu.
  • Lengo la nguzo za Uislamu kwa ujumla.
Aweze kueleza maana ya Ibada katika Uislamu.
  • Awafahamishe wanafunzi kwa maelezo na kuandika ubaoni maana ya Ibada, lengo la kuumbwa mwanaadamu na lengo la kusimamisha nguzo tano za Uislamu.
  • Asisitize kuwa Muislamu anatakiwa awe katika Ibada katika kila kipengele cha maisha yake na aonyeshe ni vipi mtu atakuwa katika Ibada muda wote wa saa 24.
Kitabu cha VII (IPC)
Twahara.
  • Hadathi.
  • Aina za Hadathi.
  • Kujitwaharisha na Hadathi.
Aweze kujitwaharisha vilivyo. Awafahamishe wanafunzi maana ya Hadathi, aina za Hadathi na namna ya kujitwaharisha kutokana na Hadathi kwa matendo Kitabu cha VII (IPC)
Maiti ya Kiislam.
  • Yaliyolazima kufanyiwa maiti.
  • Kuosha.
  • Kukafini.
  • Kuswali.
  • Kuzika.
Aweze kutekeleza mambo yote muhimu yanayostahiki kufanyiwa maiti ya Kiislamu. Awaonyeshe wanafunzi kwa vitendo namna ya kuosha maiti, kumvesha sanda, kumswalia na kumzika. Kitabu cha VII (IPC)
AKHLAQ Mwenendo wa Muislamu katika Qur-an.
  • Kumkumbuka Allah kila wakati.
  • Kumuogopa Allah ipasavyo.
Awe na mwenendo wa Kiislamu.
  • Mwalimu aonyeshe ni vipi mtu ataweza kumkumbuka alla (s.a.w) katika masaa 24 kwa kurejea dua na dhikiri za Mtume (S. A. W) alizozileta katika nyakati mbalimbali katika saa 24.
  • Asisitize umuhimu wa kumwogopa Allah (S. W.) na kumtegemea kila wakati.
Kitabu cha VII (IPC)
Tabia ya Muumini katika Qur-an.
  • Nani Muumini.
  • (8:2-4), (49:15)
  • (23:1-11),
  • (70:19-35)
  • (25:63-77) n.k.
Awe na mwenendo wa Kiislamu. Mwalimu azipitie aya zilizochaguliwa na kudhihirisha vipengele vyenye tabia njema vilivyo bainishwa humo. Kitabu cha VII (IPC)
TAREKH Historia ya Uislamu baada ya Khalifa wanne mpaka hivi leo.
  • Yaliyopelekea kuvunjika kwa Dola ya Kiislamu.
  • Mgawanyiko wa Waislamu na chanzo cha kundi la Shia.
  • Kuibuka kwa kundi la Sunni.
  • Juhudi za watu binafsi na vikundi katika kuhuisha Uislamu.
  • Uislamu ulivyoingia Afrika Mashariki.
  • Historia fupi ya Uislamu hapa Tanzania.
Awe na ari ya kusimamisha Dola ya Kiislamu katika jamii. Mwalimu kwa muhtasari aeleze historia ya Uislamu baada ya Khalifa wanne mpaka hivi leo akizingatia matukio muhimu na mafundisho yanayopatikana humo. Kitabu cha VII (IPC)

Muhtasari kwa madarasa mengine

Home Darasa la Kwanza Darasa la Pili Darasa la Tatu Darasa la Nne Darasa la Tano Darasa la Sita

Muhtasari huu umetayarishwa na Islamic Propagation Centre, S. L. P. 55105, Dar es salaam, Tanzania